ASASH GENERAL TRADERS

ASASH GENERAL TRADERS

Saturday, February 21, 2015

BALLOTELI AJIBU MAPIGO YA GERRALD

Bao pekee la mshambuliai mtukutu Mario Ballotel liliisaidia timu yake kuweza kuibuka na ushindi wa goli hilo moja dhidi ya wageni wao Besikitas katika round ya kwanza ya 32 bora Europa League, bao hilo lilipatikana mnamo dakika ya 85 kipindi cha pili kwa njia ya Penalt.

Licha ya bao hilo kupatikana Steven Gerrard amemuonya mshambuliaji huyo aliykipiga wakati huo akiwa na Inter Milan, Ac Milan, Manchester City na pia Liverpol kwasasa kuwa hakuonesha heshima kwa Captain wake Henderson kufanya uamuzi wa kumpokonya mpira na kupiga penalt maana alifanya kitu ambacho hakikuwa sahihi, na hayo yalionekana mara baada ya winga Jordan Ibe kufanyiwa faulo eneo la hatari.

Mshambuliaju huyo alimpokonya mpira Jordan Henderson mkononi huku akizinguana na Daniel Strurridge kabla hajaenda kupiga.

Captai mstaafu Steven Gerrard alisema
“Henderson ni kapteni na Ballotel alimuoneshea heshima isiyo sawa kumpokonya mpira, sharia ni sharia tu” Gerrard alisema na pia aliongezea kwa kumpongeza Ballotel kufunga hiyo penalt na kuipa ushindi Liverpool
lakini akisisitiza kusema sio vizuri kuwaona wachezaji wakibishana uwanjani na kumaliza akisema “Nadhani Henderson amekubaliana na hali vizuri”

15

BALOTELLI AJIBU MAPIGO YA GERRARD

Baada ya hapo awali nahodha wa klabu ya Liverpool Steven Gerrard kusema kuwa kitendo cha mshambuliaji wa klabu hiyo Mario Balotelli kuchukua mpira kwa kiungo Jordan Henderson na kwenda kupiga penati ni utovu ni nidhamu,mshambuliaji huyo amejibu mapigo hayo ili kuondoa mzozo uliozagaa katika sehemu mbalimbali.
Balotelli amesema anamshukuru Henderson kwa kumpa nafasi ile na kufanikiwa kuleta ushindi muhimu kwa timu.
Liverpool iliibuka na ushindi wa 1-0 dhidi ya Besiktas katika mechi iliyopigwa jana Anfield ikiwa ni mechi ya michuano ya europa ligi hatua ya mtoano huku goli hilo lililofungwa dakika ya 85 na Balotelli kwa mkwaju penati likizua utata ikionekana kuwa mchezaji huyo raia wa italia alimpokonya mpira Jordan Henderson ili akapige penati.
Hii imeshawahi kutokea katika klabu ya Everton walipokuwa wanacheza dhidi ya Westbromich January 19 mwaka huu katika uwanja wa Goodson Park ambapo Kevin Mirallas alimpokonya mpira Leighton Baines na na kwenda kupiga penati na matokeo yake akakosa.
Ushindi huu wa Liverpool unawapa nguvu ya kusonga mbele katika michuano hiyo wakiwa wanasubiria mechi ya marudiano itakayopigwa tarehe 26/2/2015 kule mjini Instanbul nchini Uturuki.
Aidha goli hilo la Balotelli ni la nne kuifungia klabu hiyo tangu asajiliwe msimu huu kwa ada ya Paundi milion 16 akitokea nchini Italia katika klabu ya AC Milan.

No comments:

Post a Comment