ASASH GENERAL TRADERS

ASASH GENERAL TRADERS

Monday, August 8, 2016

MAVUGO AWAITA WANASIMBA TAIFA LEO

Mchezaji wa kimataifa wa Burundi Laudt Mavugo amewaambia wanasimba wajitokeze kwa wingi kushuhudia mchezo wa kirafiki wa leo dhidi ya AFC leopards.

SIMBA SC KIBOKO YAO


Simba damu fans


KIKOSI CHA VIONGOZI WA SIMBA SIKU YA SIMBA DAY 2015
Simba hatetereki, Simba hutamba hata Jangwani achilia mbali milimani na kwenye nyika ambako yeye ni mfalme. Simba hupambana, Simba huwinda bila kukata tamaa hata anapokua mgonjwa. Wajuzi husema hata akonde vipi, Simba hafanani na mbwa.

Ndugu wanasimba, hilo linadhihirishwa na sapoti ya hali ya juu ambayo tumekua tukiitoa kwa timu yetu kwenye kila aina ya nyakati. Tumekua wamoja pamoja na changamoto za hapa na pale, tukipasua milima na mabonde na hatimaye nuru imeanza kuonekana.

Tupo katika hatua nzuri ya maendeleo ya kweli. Hatua ya mabadiliko ya mfumo wa klabu yetu ambao nia na madhumuni ni kuifanya iweze kujitegemea kiuchumi. Tena uchumi ulio thabiti na imara katika dunia ya sasa.

Pamoja na ukweli kwamba kwa miaka ya hivi karibuni tumeikosa ile Simba tunayoijua, lakini walau uwanja wetu wenyewe upo katika hatua nzuri tu na ninaweza kukuhakikishia kwamba utakamilika muda si mrefu. Tuwe na uwanja wa mazoezi wa kwetu wenyewe, ni kitu ambacho kilishindikana kwa kipindi kirefu na ni kitu ambacho hata wenzetu wengi wameshindwa kufanya.

Si nia yangu kueleza hayo leo, nia yangu ni kuwakumbusha jambo hili ambalo pia limekua likidhihirisha kwamba Simba ni klabu ya watu makini. SIMBA DAY ni sikukuu yetu Wanasimba ambayo naweza kusema ni tamasha kubwa la klabu katika ukanda wetu huu wa Afrika Mashariki.

Hakuna timu yoyote ambayo imeweza kuwa na utaratibu kama huu, na hiki ni kitu ambacho wanasimba tunapaswa kujivunia. Ni kitu kinachotuunganisha sisi, viongozi wetu na wachezaji wetu.

Hii ni Simba Week, ambapo shughuli nyingi za kuelekea kwenye kilele cha siku yetu zinafanyika. Tunafanya usafi, tunatembelea wagonjwa, tunatoa misaada na mambo mengine mengi kwa jamii yetu. Lakini kilele cha yote haya ni Agosti 8 pale uwanja wa taifa

Kilele cha siku hii ni mechi kati ya Simba na FC Leopards kutoka Kenya lakini itatanguliwa na mambo mengi kama utambulisho wa jezi zetu mpya ambazo pia zitakua zikiuzwa pale uwanjani.

Tutazitambua namba za wachezaji wetu watazozitumia kwenye msimu mpya,
Lakini pia tutakiona kikosi chetu chote siku hiyo. Wachezaji wapya wakiwemo wale wa kimataifa pamoja na wazamani ambao kwa pamoja wataunda kikosi kipya cha Simba chenye kila aina ya matumaini, watatambulishwa mbele ya Wanasimba.

Hii ni fursa ya pekee ambayo inapatikana mara moja tu kwa mwaka. Fursa ya kuwaona wachezaji wote wakitambulishwa na kisha kuwaona uwanjani wakimenyana na AFC Leopards.

Kama wewe ni mwanasimba, njoo uwanja wa taifa Agosti 8 ili uwe sehemu ya Simba itakayoandika historia mpya.
Njoo uwe sehemu ya vuguvugu la mabadiliko ya mfumo wa uendeshaji wa vilabu, mfumo ambao ni sisi tunaokwenda kuuanzisha hapa nchini. Tayari wapinzani wanaweweseka na wanatamani kuiga kwa sababu wanajua Simba akiwa imara anatisha kiasi gani.

Njoo tuongee ya kwetu, tuburudike kwa pamoja kama familia kwa sababu kutakua na burudani nyingi na show zilizoandaliwa na uongozi kwa ajili yetu.
Njoo tujivunie kua Simba,

Simba Nguvu Moja


Imeandikwa na Ally shatry (Bab chicharito)
06Aug2016

Saturday, July 30, 2016

MO AIBUKIA MAZOEZINI SIMBA SC


Mfanyabishara kijana na maarufu ndani na nje ya nchi, Mohammed Dewji ‘MO’ ambaye ametajwa kutaka kuwekeza kwenye Klabu ya Simba kwa kutoa Sh bilioni 20, jana aliibuka kwenye mchezo wa kirafiki wa timu hiyo dhidi ya Moro Kids.

Katika mchezo huo uliochezwa kwenye Uwanja wa Chuo cha Biblia Highlands, Morogoro uliishuhudia Simba ikishinda mabao 2-0 dhidi ya wenyeji hao na kuwa ushindi wa pili mfululizo baada ya wiki iliyopita kuifunga Polisi Moro mabao 6-0.

Mabao ya Simba yalifungwa na Ibrahim Ajib dakika ya 20 akipokea pasi ya Shiza Kichuya na la pili lilifungwa na Danny Lyanga dakika ya 69 akiunganisha pasi ya Mohammed Ibrahim.

Katika hali isiyokuwa ya kawaida, mashabiki waliojitokeza uwanjani hapa muda wote wa mchezo walikuwa wakiimba nyimbo za kuushinikiza uongozi umpe timu MO.
Mashabiki hao walisikika wakiimba: “Mo tumpe timu.”


Baada ya mchezo huo Kocha Joseph Omog wa Simba alisema, amefurahishwa na uwezo ulioonyesha na wachezaji wake huku akidai wapinzania wao walikuwa katika kiwango bora

Friday, July 29, 2016

MO KUWEKEZA BILIONI 20 SIMBA SC,,WANACHAMA WACHEKELEA

MOhammed Dewji 'MO' amejitokeza hadharani na kukiri yupo tayari kufanya uwekezaji wa bilioni 20 kwa klabu ya Simba endapo wanachama wa klabu hiyo wataridhia.

Mo amekuwa akihusishwa na kutaka kufanya uwekezaji huo mkubwa ndani ya Simba huku baadhi ya wanachama wa klabu hiyo wakionekana kutokuwa tayari kutokana na sababu zao binafsi.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisi kwake jijini Dar es Salaam MO alisema kinachomvutia kufanya uwekezaji huo mkubwa kwa Simba ni mapenzi aliyonayo kwa klabu hiyo huku akijaaliwa kipato kikubwa na Mungu.

"Simba naipenda toka moyoni, niliwahi kuidhamini miaka ya nyuma na tulifanya vizuri sana katika michuano ya kimataifa kila mwanasimba analijua," alisema MO.

Aidha Mo alisema bajeti ndogo ya Simba ndiyo inayoifanya klabu hiyo kushindwa kushindana katika solo la usajili na kutowalipa vizuri wachezaji kama ilivyo kwa Yanga na Azam.

Wakati huo huo MO alisema ndani ya miaka mitatu endapo atakubaliwa  kufanya uwekezaji atajenga kiwanja bora cha mpira, hosteli, Gym na kuajiri kocha mwenye vigezo.

Simba inatarajiwa kufanya mkutano mkuu wa wanachama utakaojadili juu ya uwendeshwaji wa klabu hiyo siku ya Jumapili katika Bwalo la maofisa wa Polisi Oysterbay.

Wakati huohuo,,baadhi ya mashabiki wa Simba SC wamefurahishwa na hatua hiyo ya mfanyabiashara huyo.

Monday, February 22, 2016

BANDA; ILIKUWA NGUMU ZAIDI KUPAMBANA TUKIWA PUNGUFU

Kiungo mshambuliaji wa Simba Sc Abdi Banda, amesema kuwa kupoteza mchezo dhidi ya Yanga ilikuwa dhahiri kuanzia dakika ya 25 baada ya muamuzi Jonasia Rukiyaa kumuadhibu kwa kadi nyekundu.

Abdi Banda juzi alitolewa mapema katika mchezo ambao ulikuja kuwa wa hovyo baada ya kumgusa kwenye bega mshambuliaji wa Yanga Donald Ngoma,.

Katika hatua nyingine,ungozi wa Simba SC umewapa mapumziko ya muda mfupi wachezaji wake kabla ya kuivaa Mbeya City  katika mchezo utakaopigwa Machi 6.

Friday, March 6, 2015

7000 KUONA SIMBA DHIDI YA YANGA

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limetangaza viingilio vya mchezo wa siku ya jumapili kati ya Simba SC na Young African utakaofanyika kwenye dimba la Uwanja wa Taifa kuanzia majira ya saa 10 kamili za jioni.


Mchezo huo utachezeshwa na mwamuzi Martin Saanya kutoka Morogoro, akisaidiwa na Soud Lila (DSM) mshika  kibendera wa kwanza, Florentina Zabron (Dodoma) mshika kibendera wa pili, Mwamuzi wa akiba Israel Mjuni (DSM), na kamisaa wa mchezo ni Ame Santimeya (DSM).

Viingilio vya mchezo huo,  VIP A sh. 40,000, VIP B sh. 30,000, VIP C sh. 20,000, Rangi ya Machungwa (Orange) sh. 10,000, huku Rangi ya Bluu na Kijani ikiwa ni sh. 7,000.

Tiketi zitaanza kuuzwa keso (jumamosi) saa 2 kamili asubuhi katika vituo vya,  Karume (Ofisi za TFF), Mgahawa wa Steers (Posta Mpya), Oilcom (Buguruni), BigBon (Kariakoo),  Olicom (Ubungo), Dar Live (Mbagala), Uwanja wa Uhuru, Kivukoni (Ferry) na Makumbusho (kituo cha mabasi).

Magari yenye vibali maalum ndiyo yatakayoruhusiwa kuingia ndani ya uwanja siku ya jumapili kwa kupitia barabara ya Mandela na Uwanja wa Uhuru, barabara ya Chang'ombe itafungwa kuanzia saa 12 kamili asubuhi.

TFF inawaomba, wapenzi, washabiki na wadau wa mchezo kununua tiketi katika vituo vilivyotajwa ili kuepuka kuuziwa tiketi bandia, ili kuimarisha ulinzi na usalama wa mchezo, mashabiki wenye mabegi, silaha, vilevi na chupa za maji hawataruhusiwa kuingia navyo uwanjani.


Aidha, katika mchezo huo TFF itatoa ujumbe maalum kupitia kwa wachezaji kuhamasisha juhudi za Taifa za kuzuia mauaji dhidi ya watu wenye ulemavu wa ngozi (Albino).

Monday, March 2, 2015

KILOMONI ; MCHEZAJI PEKEE KUWAUA YANGA 4 KWA MIGUU YAKE


Mzee Hamisi Ally Kilomoni, mchezaji wa zamani wa Sunderland anayekumbukwa na Yanga kwa jinsi alivyokuwa anapachika mabao dhidi yao. Picha kwa hisani ya Bin Zubeiry.
 
SUNDERLAND, ambayo wakati huo ilikuwa ikishikilia ubingwa wa kandanda wa Afrika Mashariki ‘Allsopps Cup’ pamoja na ubingwa wa Taifa, Jumapili ya Mei Mosi, 1966 iliinyoa Yanga bila maji kwa kuifunga magoli 4-0 katika Uwanja wa Ilala, mbele ya waheshimiwa Makamu wa Pili wa Rais, Rashid Mfaume Kawawa, Mawaziri, Mabalozi, Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Selemani Kitundu na maelfu ya watazamaji waliojazana hapo. Mara baada ya mchezo mashabiki wa Sunderland walilipuka kwa mayowe ya furaha huku wakiitania Yanga kuwa ni ‘Four-Four’ kwa kufungwa magoli manne bila majibu. Wakati huo gari za Peugeot 404 kutoka Ufaransa ndiyo kwanza zilikuwa zinaingia nchini.
Hii ilikuwa ni fainali ya kugombea Kombe la NUTA lililotolewa kushindaniwa maalum kwa sherehe za Sikukuu ya Wafanyakazi Duniani, yaani May Day.
Mpira ulianza huku mvua ikinyesha na upepo mwingi ukivuma. Yanga ndio walioanza kuingia uwanjani wakipitia mlango usiostahili kupitiwa, lakini yote hiyo haikufaa kitu, kwani goli nne kwa yai ziliamua nani bingwa wa soka. Kipigo hicho kilikuwa kama cha kulipa kisasi baada ya Sunderland kufungwa 5-4 na Yanga hapo Machi Mosi katika fainali ya Kombe la Nyota.
Timu zote zilitambulishwa kwa mgeni wa heshima, Makamu wa Pili wa Rais, Rashid Kawawa. Baada ya hapo mpira ukaanza huku Sunderland, Sanda au Abidjan, kama walivyokuwa wakiitwa, wakicheza mchezo wa haraka haraka (quick game) ili kuwachosha mabeki wa Yanga.
Zilipotimu dakika tatu tu mpira ukawa miguuni mwa Asmat, winga wa kushoto wa Sunderland, na hapo ikatumika ‘one touch’, akamlamba chenga Abuu Mapyopyo wa Yanga na kumpasia Hamisi Kilomoni, ambaye alimzungusha Athumani Kilambo wa Yanga na kisha akampasia Mustafa Choteka, naye bila kuchelewa akammegea Haji Lesso, ambaye alifumua shuti kali la ‘mwana-ukome’ huku akiwa kafumba macho. Alipofumbua akapashwa habari kwamba mpira umetikisa nyavu za Yanga.
Haukupita muda mrefu Mustafa aliutupa mpira hadi kwa Haji, ambaye kwa mara nyingine tena bila kufanya makosa akafunga goli la pili kwa Sunderland. Mpira uliendelea huwa wa vuta-nikuvute hadi kilipomalizika kipindi cha kwanza.
Wakati wote huu Sunderland walikuwa wakitumia staili zao mpya za ‘Abidjan’. Watu wengi walikuwa hawajui jinsi staili za Abidjan zinavyochezwa, lakini siku hiyo walijionea wenyewe, yaani mfungaji magoli huwa mmoja tu naye ni ‘Insaidi’ au ‘sentafowadi’. Ndivyo ilivyokuwa siku hiyo, kwani Haji ndiye aliyefunga magoli mengine mawili katika kipindi cha pili na kuipatia timu yake ushindi mnono dhidi ya mahasimu wao wakubwa, Yanga.
Siku hiyo timu zilipangwa hivi: 
YANGA: Saad Mohammed Songambele, Abuu Mapyopyo, Omari Kapera, Athumani Kilambo, Juma Washokera, Awadh Gessani, Kassim Lengwe, Mfamau, Peter Mandawa, Mtumwa Mgeni, Mwinyiamiri Mwinyimadi.
SUNDERLAND: Mbaraka Salum Magembe, Tayari Mussa, Mussa Libabu, Yussuf Omari Kimimbi, Gilbert Mahinya, Adam Athmani, Abdu Rashid Kibunzi, Hamisi Kilomoni, Haji Lesso, Astmati, Mustafa Choteka, Arthur Mambetta.
Mwamuzi alikuwa Marijani Shabani Marijani aliyesaidiwa na Gration Matovu kutoka Tanga. Kamisaa alikuwa Balozi B.J. Maggid, aliyekuwa Rais wa FAT, wakati mgeni rasmi alikuwa Rashid Mfaume Kawawa, Makamu wa Pili wa Rais.

NB: Makala haya ni kutoka kwenye muswada wa kitabu cha 'VUTA-NIKUVUTE: SIMBA NA YANGA' cha mwandishi Daniel Mbega, ambacho kiko katika hatua za mwisho kuchapishwa. Unaweza kuwasiliana naye kwa simu +255 715 070109 au brotherdanny5@gmail.com

Thursday, February 26, 2015

CHIDY BENZ AHUKUMIWA


Msanii hip hop, Rashid Makwiro 'Chid Benz' amehukumiwa miaka miwili kwenda jela.



Hukumu hiyo imetolewa leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Kisutu jijini Dar es Salaam ambako kesi yake ya kukamatwa na madawa ya kulevya ilikuwa inasikilizwa.

Hukumu ilikuwa ni adhabu ya miaka miwili jela au kulipa faini ya Sh 9,000,000 ambayo aliilipa baada ya watu wake kujitokeza na kukamilisha hilo na sasa Chid Benz.

Kesi yake hiyo iliyoendeshwa kwa wiki kadhaa, ilitokana na msanii huyo kukamatwa na madawa ya kulevya kwenye Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere akiwa njiani kwenda mjini Mbeya kwa ajili ya shoo.

Chid Benz alikiri madawa aliyokamatwa nayo kwenye mfuko wa shati yalikuwa yake.

Sunday, February 22, 2015

BREAKING NEWSS , CHRISTOPHER ALEX AFARIKI DUNIA

Kiungo wa zamani wa Simba Sc Christopher Alex Massawe Amefariki Dunia... Habari zaidi zitafuatia muda mfupi ujao!

PENALTI ILIYOIPA KIBURI SIMBA SC YAZIMIKA GHAFLA

Aliyekuwa kiungo nyota wa Simba, Christopher Alex Massawe, amefariki dunia.


Alex amefariki dunia kwa mjini Dodoma ikiwa ni baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Dada wa marehemu aliyejitambulisha kwa jina la Mama Maembe amesema Alex amefariki dunia leo saa 3 asubuhi.

Tayari taratibu za mazishi zimeanza kufanywa na imeelezwa Alex atazikwa mjini humo.


Alijulikana kwa ubora wake katika ukabaji na kuichezesha timu. Lakini pia atakumbukwa kwa kuwa mchezaji aliyepiga penalti ya mwisho iliyoivua ubingwa Zamalek na kuipeleka Simba kucheza Kombe la Ligi ya Mabingwa Afrika 2003, hatua ya makundi.

Saturday, February 21, 2015

BALLOTELI AJIBU MAPIGO YA GERRALD

Bao pekee la mshambuliai mtukutu Mario Ballotel liliisaidia timu yake kuweza kuibuka na ushindi wa goli hilo moja dhidi ya wageni wao Besikitas katika round ya kwanza ya 32 bora Europa League, bao hilo lilipatikana mnamo dakika ya 85 kipindi cha pili kwa njia ya Penalt.

Licha ya bao hilo kupatikana Steven Gerrard amemuonya mshambuliaji huyo aliykipiga wakati huo akiwa na Inter Milan, Ac Milan, Manchester City na pia Liverpol kwasasa kuwa hakuonesha heshima kwa Captain wake Henderson kufanya uamuzi wa kumpokonya mpira na kupiga penalt maana alifanya kitu ambacho hakikuwa sahihi, na hayo yalionekana mara baada ya winga Jordan Ibe kufanyiwa faulo eneo la hatari.

Mshambuliaju huyo alimpokonya mpira Jordan Henderson mkononi huku akizinguana na Daniel Strurridge kabla hajaenda kupiga.

Captai mstaafu Steven Gerrard alisema
“Henderson ni kapteni na Ballotel alimuoneshea heshima isiyo sawa kumpokonya mpira, sharia ni sharia tu” Gerrard alisema na pia aliongezea kwa kumpongeza Ballotel kufunga hiyo penalt na kuipa ushindi Liverpool
lakini akisisitiza kusema sio vizuri kuwaona wachezaji wakibishana uwanjani na kumaliza akisema “Nadhani Henderson amekubaliana na hali vizuri”

15

BALOTELLI AJIBU MAPIGO YA GERRARD

Baada ya hapo awali nahodha wa klabu ya Liverpool Steven Gerrard kusema kuwa kitendo cha mshambuliaji wa klabu hiyo Mario Balotelli kuchukua mpira kwa kiungo Jordan Henderson na kwenda kupiga penati ni utovu ni nidhamu,mshambuliaji huyo amejibu mapigo hayo ili kuondoa mzozo uliozagaa katika sehemu mbalimbali.
Balotelli amesema anamshukuru Henderson kwa kumpa nafasi ile na kufanikiwa kuleta ushindi muhimu kwa timu.
Liverpool iliibuka na ushindi wa 1-0 dhidi ya Besiktas katika mechi iliyopigwa jana Anfield ikiwa ni mechi ya michuano ya europa ligi hatua ya mtoano huku goli hilo lililofungwa dakika ya 85 na Balotelli kwa mkwaju penati likizua utata ikionekana kuwa mchezaji huyo raia wa italia alimpokonya mpira Jordan Henderson ili akapige penati.
Hii imeshawahi kutokea katika klabu ya Everton walipokuwa wanacheza dhidi ya Westbromich January 19 mwaka huu katika uwanja wa Goodson Park ambapo Kevin Mirallas alimpokonya mpira Leighton Baines na na kwenda kupiga penati na matokeo yake akakosa.
Ushindi huu wa Liverpool unawapa nguvu ya kusonga mbele katika michuano hiyo wakiwa wanasubiria mechi ya marudiano itakayopigwa tarehe 26/2/2015 kule mjini Instanbul nchini Uturuki.
Aidha goli hilo la Balotelli ni la nne kuifungia klabu hiyo tangu asajiliwe msimu huu kwa ada ya Paundi milion 16 akitokea nchini Italia katika klabu ya AC Milan.