Baada ya kukaa nje ya uwanja takriban wiki moja sasa kutokana na majeraha waliyoyapata katika michezo ya muendelezo wa ligi kuu Tanzania bara, wachezaji wa SSC, Henry Joseph (Shindika) na Said Nassor Chollo , wameanza rasmi mazoezi leo asubuhi na jioni kwenye uwanja wa mazoezi wa Kinesi jijini Dar.
Hii ni katika kujiandaa na mchezo wa mwisho wa wiki hii dhidi ya Ruvu Shooting.Utaopigwa katika uwanja mkuu wa Taifa.
Wakati huohuo, mchezaji Amry Kiemba anaendelea vizuri baada nae kupata majeraha katika mchezo uliopita dhidi ya JKT Ruvu.
No comments:
Post a Comment