ASASH GENERAL TRADERS

ASASH GENERAL TRADERS

Thursday, February 6, 2014

SIMBA WAENDA TANGA LEO

Timu ya soka ya Simba Sc, ipo njiani kuelekea mkoani Tanga tayari kabisa kuwavaa wanajeshi wa Jkt Mgambo.

Katika mechi hiyo itakayochezwa uwanja wa mkwakwani, Kikosi hicho cha kocha Zdravko Lugarusic kitalazimika kucheza kufa au kupona ili kuweza kupata points tatu muhimu , baada ya Jana kuacha points mbili katika uwanja wa Jamhuri,.

Simba. Jana ililazimishwa sare na Mtibwa Sugar, baada ya kuwa nyuma kwa goli 1-0 kwa takriban dakika 40, baada ya Mussa Hassan Mgosi, kuitikisa Ngome ya ulinzi ya Simba Sc mnamo dakika ya 9 tu ya mchezo huu,.

Shukrani kwa mshambuliaji Amissi Tambwe ambaye alifanya kazi ya ziada kipindi cha pili, kuisawazishia kikosi hicho cha Msimbazi.

No comments:

Post a Comment