ASASH GENERAL TRADERS

ASASH GENERAL TRADERS

Friday, February 28, 2014

NI REKODI TU NDIYO INAYOIBEBA AL AHLY DHIDI YA YANGA HAPO KESHO

Kikosi cha mabingwa wa soka Tanzania bara Dar Young Africans, kesho kinajitupa katika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam kuwavaa Mabingwa watetezi wa Afrika National Al Ahly.

Katika mechi hiyo inayosubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa timu hiyo, Yanga itaingia dimbani huku ikiongozwa na nyota wa kimataifa mwenye uchu wa magoli Emanuel Arnold Okwi.
Ikumbukwe kuwa katika mechi sita ambazo Yanga imefanikiwa kucheza dhidi ya AL Ahly haikuwahi kushinda mchezo wowote zaidi ya kutoa sare katika michezo miwili.

Yanga iliyo katika kiwango cha hali ya juu hivi sasa,inahitaji ushindi wa aina yoyote dhidi ya miamba hiyo ya Afrika ili kujiwekea mazingira mazuri ya kufuzu raundi ya pili ya michuano hiyo.

No comments:

Post a Comment