ASASH GENERAL TRADERS

ASASH GENERAL TRADERS

Friday, February 28, 2014

SIMBA; TUTAIDUWAZA RUVU SHOOTING ILI HESHIMA YETU IRUDI

Kikosi kilichokosa muelekeo wa kutwaa ubingwa wa Tanzania bara timu ya Simba Sc ,kimeapa kuwa lazima izipate alama zote tatu katika mechi inayofuata dhidi ya Ruvu Shooting.

Wakiongea na blog ya Simba Platinum Supporters mshambuliaji wa kimataifa wa burundi Amissi Tambwe na beki ya kati Donald Musoti, wamesema kuwa wanafahamu kuwa wanachama na mashabiki wa Simba wamekata tamaa na timu yao lakini hilo lisiwavunje moyo kwani timu iko katika hali nzuri na watacheza vizuri zaidi ili kuweza kuondoka na alama zote.

Simba iliyo katika kiwango kisichoridhisha ,inahitaji ushindi wa aina yoyote ile ili kuweza kujipalilia nafasi nzuri zaidi itakayoifanya iweze kushiriki michuano ya Afrika mwakani.

Wakati huo huo, mchezo utakaofanyika jumapili dhidi ya Ruvu Shooting,huenda ukashuhudia urejeo wa Captain Massoud Nassor Chollo baada ya afya ya mchezaji huyo kuimarika.

No comments:

Post a Comment