ASASH GENERAL TRADERS

ASASH GENERAL TRADERS

Wednesday, February 26, 2014

TWAHA MAJERUHI YAANZA UPYA

Kiungo mshambuliaji wa timu ya Simba SC ya mitaa ya Msimbazi Ibrahim Twaha Shekua maarufu kama Neymar wa msimbazi,anapitia katika kipindi kingine kigumu katika maisha yake ya soka baada ya kurejea tena maumivu katika eneo la paja katika mguu wake.

Mchezaji huyo ambaye alikuwa na hamu ya kurudi uwanjani ili kumthibitishia kocha wa sasa wa Simba Zdravko alugarusic kuwa yuko sawa,inabidi aongezewe wiki zaidi kabla ya kurejea tena uwanjani.
Ikumbukwe kuwa Twaha aliumia katika mazoezi ya kujiandaa na pambano la Yanga lililoisha kwa sare ya 3-3.

Hili litakuwa pigo lingine ambalo linaifanya klabu hiyo kuanza upya baada ya juzi kumpoteza mshambuliaji Zahoro Pazi ambaye naye kwa sasa ni majeruhi .

No comments:

Post a Comment