ASASH GENERAL TRADERS

ASASH GENERAL TRADERS

Monday, January 27, 2014

SIMBA,AZAM,MBEYA CITY,YANGA ZAANZA VEMA LIGI KUU TANZANIA BARA




TIMU kongwe ya Simba jana iliuanza vyema mzunguko wa pili wa ligi kuu ya soka ya 
Tanzania Bara baada ya kuichapa Rhino Rangers bao 1-0 katika mechi iliyopigwa 
kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Bao pekee na la ushindi la Simba lilifungwa na mshambuliaji machachari, Ramadhani 
Singano 'Messi katika dakika ya 14.
Simba ilifanikiwa kupata mabao mengine mawili, moja katika kila kipindi, lakini 
yalikataliwa na mwamuzi Andrew Shamba kwa madai kuwa yalitendeka madhambi 
kabla ya mpira kujaa wavuni.
Simba ilipata nafasi nyingine nzuri ya kufunga bao kipindi cha pili baada ya 
kuzawadiwa penalti, kufuatia beki mmoja wa Rhino kuunawa mpira ndani ya eneo la 
hatari, lakini shuti la Messi lilimlenga kipa Charles Mpinuki wa maafande hao wa 
jeshi.


Katika mechi zingine za ligi hiyo zilizochezwa mwishoni mwa wiki iliyopita, mabingwa 
watetezi Yanga waliichapa Ashanti mabao 2-1 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es 
Salaam.
Nayo Azam iliendelea kujichimbia nafasi ya pili katika msimamo wa ligi hiyo baada ya 
kuichapa Mtibwa Sugar bao 1-0 kwenye uwanja wa Chamazi wakati Mbeya City 
iliitambia Kagera Sugar ugenini baada ya kuichapa bao 1-0 kwenye Uwanja wa 
Kaitaba.
Katika mechi zingine za ligi hiyo zilizochezwa mwishoni mwa wiki iliyopita, Coastal 
Union ilitoka sare ya bao 1-1 na JKT Oljoro kwenye Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.

No comments:

Post a Comment