UCHAMBUZI wa haraka ni kwamba, Chelsea imeziweka wazi mno mbio za ubingwa wa Ligi Kuu ya England, kufuatia ushindi wake wa bao 1-0 dhidi ya wenyeji Manchester City, Uwanja wa Etihad usiku huu.
Shukrani kwake mfungaji wa bao hilo pekee Ivanovic dakika ya 32 na sasa Chelsea inatimiza pointi 53 sawa na Manchester City iliyo nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi kwa wastani wake mzuri wa mabao.
Matokeo hayo yanakuwa faraja zaidi kwa Arsenal ambayo sasa inatuliza roho kileleni mwa Ligi Kuu kwa pointi zake 55, baada ya timu zote hizo kucheza mechi 24.
Tumewashikisha adabu: Ivanovic akishangilia baada ya kuifungia Chelsea bao pekee la ushindi usiku huu
Kupaki basi? Siyo mimi: Mourinho akionekana mwenye furaha na matokeo ya timu yake,huku Manuel Pellegrini akifoka
Edin Dzeko wa City na Nemanja Matic wa Chelsea
Kipa Petr Cech na beki wake Gary Cahill wakijaribu kuondosha mpira hatarini kabla Alvaro Negredo hajaupata
Martin Demichelis na Eden Hazard
David Silva alipiga nje hapa
Hazard akiwatoka Pablo Zabaleta na Demichelis
No comments:
Post a Comment