ASASH GENERAL TRADERS

ASASH GENERAL TRADERS

Thursday, October 2, 2014

TFF YAAGIZA NI LAZIMA VILABU VIKATWE ASILIMIA TANO


Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amesema ni lazima klabu zikatwe fedha zao za udhamini.

TFF iliagiza klabu zote 14 za Ligi Kuu Bara, zikatwe fedha zao za udhamini kutoka Vodacom na Azam TV.
Agizo hilo, liliamsha hisia za klabu ambazo zilisisitiza kwamba haziwezi kukubali hali.
Hali iliyosababisha Mbeya City na Mtibwa Sugar, kutishia kwenda mahakamani.
Akizungumza leo, Malinzi alisema lazima fedha hizo zikatwe kwa ajili ya mfuko wa maendeleo ya soka.
"Hilo suala la kukatwa fedha limeishapita, ni agizo na lazima litekelezwe," alisema Malinzi.
 

Imehamishwa toka kwa Saleh Ally

No comments:

Post a Comment