ASASH GENERAL TRADERS

ASASH GENERAL TRADERS

Sunday, February 23, 2014

TWAHA AANZA RASMI MAZOEZI KESHO,HUGO KITAAAMBO

Wachezaji wawili wenye kasi ya ajabu Ibrahim Twaha Shekuwa maarufu kama Neymar wa msimbazi pamoja na Abdallah Seseme Hugo wanarejea rasmi kikazi zaidi baada ya kuwa nje ya uwanja takriban miezi mitatu.

Twaha ambaye alipata maumivu ya paja baada ya kuanguka vibaya kwenye mazoezi ambapo Simba iliweka Camp ya muda kwenye uwanja wa Bamba Beach,anarejea kesho kikazi huku akiwa na hamu ya kumthibitishia kocha wa sasa wa Simba SC Zdravko Lugarusic kuwa yeye anastahili kuwemo kwenye kikosi cha kwanza.

Wakati IBRA akiwaza hayo,mwenzake Abdallah Seseme maarufu kama Hugo naye ameanza mazoezi tangu wiki iliyopita.

Ikumbukwe kuwa Hugo aliumia katika mazoezi katika uwanja wa kinesi jijini Dar es salaam.

Wakati huo huo, Simba Sc leo inatarajiwa kumkosa Ramadhan Singano Messi na kushuhudia urejeo wa Edward Christopher katika kikosi kamili cha kwanza.

No comments:

Post a Comment