ASASH GENERAL TRADERS

ASASH GENERAL TRADERS

Sunday, February 23, 2014

YANGA WAJIPIGILIA MSUMARI WA MOTO BAADA YA KUMCHEZESHA OKWI

Mabingwa wa ligi kuu Tanzania bara Dar Young Afrika, wamejiweka katika wakati mgumu baada ya kumchezesha mchezaji mwenye utata wa usajili Emanuel Okwi katika mchezo wa jana dhidi ya Ruvu Shooting.

Okwi ambaye alizuwa na shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF,alicheza mchezo wa jana na kufunga goli safi kabisa katika kipindi cha kwanza.

Ikumbukwe kuwa, TFF iliomba muongozo FIFA kuhusu nyota huyo wa Uganda The Cranes, kabla ya FIFA kuiamuru TFF Ifuatilie umakini wa usajili wa mchezaji huyo ambapo TFF hawakufanya hivyo.

Yanga, jana iliweza kufanya kufuru ya soka baada ya kuiua timu iliyoonekana ngumu ya Ruvu Shooting kwa kipigo cha kihistoria cha goli 7-0.

No comments:

Post a Comment