ASASH GENERAL TRADERS

ASASH GENERAL TRADERS

Wednesday, October 1, 2014

MDAU WA SIMBA SC ANAPOILILIA SIMBA YAKE


KAMA SHABIKI NA MWANACHANAMA WA SIMBA SPORTS CLUB MANENO HAYA YANA UKWELI NDANI YAKE??? TUTAFAKARI Kocha Julio: kuvurunda kwa Simba kuna mkono wa mtu KOCHA mwenye maneno mengi ambaye pia ni shabiki mkongwe na Simba, Jamhuri Kihwelu ‘Julio’ ameshindwa kuzuia hisia zake na kudai kwamba matokeo inayopata timu hiyo kwenye Ligi Kuu Bara yana mkono wa mtu. Julio, ambaye amepata mafanikio akiwa na Simba kama mchezaji na kocha, alidai kuna baadhi ya viongozi wajuaji wanaoingilia uhuru wa benchi la ufundi lililoko chini ya Mzambia, Patrick Phiri. Ingawa Phiri amekataa kuzungumzia hilo, Julio amesisitiza kwamba ana uzoefu na kocha huyo kwani aliwahi kufanya naye kazi Simba na anaelewa hali halisi huku akidai kwamba upole wake unamgharimu katika baadhi ya mambo. Simba imecheza mechi mbili za Ligi dhidi ya Coastal Union walipotoka sare ya 2-2 na baadaye wakatoka sare nyingine ya 1-1 dhidi ya timu iliyosajili kikosi cha bei chee Polisi Morogoro. Mechi zote Simba imecheza Uwanja wa Taifa ambao ndiyo wa kisasa zaidi nchini. Phiri akijibu tuhuma hizo kwa kifupi alisema: “Sipangiwi timu nafanya kazi na benchi la ufundi, lakini viongozi wa timu kubwa kama Simba wana mambo mengi, haya matokeo ni sehemu ya mchezo haina haja ya kupaniki. Timu itakaa vizuri, kilichopo hapa ni viongozi kujenga timu kwa mfumo wa ligi nzima, kuzingatia mechi zote za msimu si kuiangalia kuifunga Yanga pekee.” Julio aliyeshindwa kwenye uchaguzi mkuu uliopita wa Simba akigombea nafasi ya Umakamu Mwenyekiti aliiambia Mwanaspoti kwamba: “Phiri aachwe afanye kazi yake, aamue nani acheze na nani akae benchi asiingiliwe. Nimefanya kazi nikiwa msaidizi wake ndani ya Simba na tulikuwa tukikumbana na matatizo kama hayo ya kupangiwa timu na watu wachache. Viongozi wafanye yao na wamuachie kocha afanye yake na si kumuingilia kwasababu ni mpole tu, hivi ni kuharibu.” “Phiri ni mwalimu profeshno, anajua kazi yake na anajua ni mchezaji gani mzuri anayeweza kucheza kwenye mchezo fulani lakini pia anajua mchezaji yupi hayuko fiti kucheza siku fulani. Naamini akiachwa afanye kazi yake Simba itabadilika,” alidai Julio ambaye kwa sasa ni kocha wa Mwadui FC inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza. Julio alienda mbali zaidi na kudai kwamba hata Kocha Zdravko Logarusic aliyetimuliwa hivi karibuni ilisababishwa na kugoma kupangiwa kikosi na baadhi ya vigogo wa Simba.

No comments:

Post a Comment